Mtaalamu wa mifumo ya biashara ya WiFi Tanzania. Tunakupa Mfumo wa Manual (Vocha) na Mfumo wa Automatic (Kiotomatiki) – Chagua mtindo unaokufaa na anza kupata mapato kila siku.
Uza WiFi Kidigitali
Maelezo ya kina: Mfumo huu unakupa uwezo wa kumiliki biashara ya WiFi ambapo wewe mwenyewe ndiye unayetengeneza vocha na kumuuza mteja. Unatumia MikroTik Router yenye mfumo wa vocha ulio tayari, na Access Point yenye nguvu ya kufikia umbali wa mita 150. Kwa mfumo huu, wewe unaamua bei za vocha kwa mujibu wa soko lako: mfano unaweza kuuza vocha ya saa 6 kwa TSh 500, vocha ya siku nzima TSh 1000, vocha ya wiki TSh 5000, au mwezi TSh 20,000. Wateja wako wananunua vocha kwako kwa pesa taslimu, M-Pesa, TigoPesa au Airtel Money, kisha unawapa namba ya vocha au unawachapishia vocha. Wao huingiza vocha kwenye ukurasa wa kuingilia (captive portal) na mara moja wanapata intaneti. Muda wa vocha ukimalizika, mfumo wa MikroTik humwondoa mteja kiotomatiki, hivyo hakuna mtu atakayetumia intaneti bure.
✅ Bei inajumuisha: MikroTik + Access Point 150m + nyaya + usaidizi wa ufungaji. Ofisi Mabibo.
Maelezo ya kina kabisa: Hii ni teknolojia ya kisasa kabisa ya biashara ya WiFi nchini Tanzania. Mfumo wa Automatic unajitegemea yenyewe. Baada ya kusakinisha, mteja anapowasha WiFi na kuungana na hotspot yako, anaelekezwa moja kwa moja kwenye ukurasa wa kuchagua package. Wateja wanachagua package: Saa 6 (TSh 500), Siku 1 (TSh 1000), Wiki 1 (TSh 5000) au Mwezi (TSh 15,000) – wewe unaweza kubadilisha bei na muda wowote. Kisha anaingiza namba yake ya simu (Tigo(Yas), Vodacom, Airtel, Halotel) na kufanya malipo kwa njia ya simu (M-Pesa, TigoPesa, Airtel Money, Halopesa) papo hapo. Baada ya malipo kuthibitishwa, intaneti inaamilishwa kiotomatiki kwenye MikroTik, mteja anapata ufikiaji mara moja. Muda ukimalizika, mfumo unamtoa mteja kwenye wateja wa router. Zaidi ya hayo, unapewa Admin Dashboard maalumu ambayo unaweza kufungua kwenye simu yako au kompyuta hata ukiwa mkoa mwingine au nchi nyingine. Kwenye dashboard utaona: jumla ya mapato, wateja walio online, wateja wote waliojiandikisha, kiasi cha pesa ulichokusanya, na kitufe cha kutoa pesa (withdrawal) wakati wowote. Unaweza pia kurekebisha packages (bei na muda) kwa kubofya tu. Mfumo huu unakufanya wewe kuwa mfanyabiashara wa kisasa ambapo huna haja ya kukaa karibu na biashara yako – unafuatilia kwa mbali na wateja wanajihudumia wenyewe.
✅ Kifurushi: MikroTik + Access Point 150m + Dashibodi + Msaada wa ufungaji + mafunzo.
Unachofanya wewe: Unatengeneza vocha kwa kutumia mfumo wa MikroTik, kisha unawauzia wateja vocha. Mteja anapoingiza vocha anapata intaneti. Unafaa kwa maeneo ambayo wateja wanakuhudumia kwa pesa taslimu au kwa utumaji wa kawaida. Hakuna gharama za kila mwezi. Una uhuru kamili wa kuweka bei na muda. Ukiwa na watu wachache, mfumo huu ni rahisi na mzuri.
Bei ya mfumo: TSh 520,000 tu.
Wateja wanajihudumia wenyewe: Wanachagua package, wanalipa kwa simu, wanapata intaneti moja kwa moja. Wewe huna haja ya kuwahudumia. Unafuatilia dashibodi yako na kuona mapato yanayoongezeka kila siku. Unaweza kuwa na biashara katika eneo moja na wewe ukiishi Dar es Salaam au mkoani mwingine. Mfumo unaofaa kwa wafanyabiashara wanaotaka kupanuka bila wafanyakazi wengi.
Bei ya mfumo: TSh 800,000 (Pamoja na dashboard ya admin).
Kifaa chenye nguvu za kudhibiti mamia ya wateja kwa wakati mmoja, na mfumo uliosanidiwa kitaalamu kulingana na mfumo uliochagua (Manual au Automatic).
Access Point ya ubora wa juu inayoweza kufikia umbali wa mita 150 katika eneo wazi. Inashughulikia maeneo makubwa kama viwanja, baa, hoteli, maeneo ya biashara.
Timu yetu inakuja kukusaidia kusanikisha vifaa, kukufundisha jinsi ya kutumia mfumo (kutengeneza vocha au kutumia dashboard). Huduma ya baada ya mauzo iko.
Miaka ya utaalamu katika mifumo ya MikroTik na biashara za WiFi Tanzania. Tunaelewa mahitaji ya wafanyabiashara wetu.
Ukiwa na swali au tatizo, timu yetu iko WhatsApp na simu. Hatuachi mteja.
Uko Dar es Salaam? Karibu ofisini kwetu Mabibo kwa maelezo zaidi na kuona mifumo ikifanya kazi.
Mabibo, Dar es Salaam
Simu / WhatsApp: +255 749 750 707
Email: duduumendez@gmail.com
Saa za kazi: Jumatatu hadi Jumamosi:. Tunakusaidia kuanzisha biashara yako kwa haraka.
Tunakuja na kukusaidia ufungaji, lakini kama una ujuzi wa msingi unaweza pia kujiweka mwenyewe. Tunatoa mwongozo kamili.
Katika eneo wazi hadi mita 150, katika maeneo yenye kuta na vizuizi inafika mita 50-80 kulingana na muundo. Inatosha kwa biashara nyingi.
Hapana. Malipo ya wateja yanaenda kwenye namba yako ya simu moja kwa moja kupitia M-Pesa, TigoPesa, Airtel Money, n.k. Kwenye dashboard unaona mapato yote.
Kwenye dashboard yako kuna kitufe cha "Withdraw". Unabofya na pesa zako zote (baada ya kukatwa gharama ndogo ya uendeshaji) zinatupwa kwa namba yako ya simu.
Ndiyo, vifaa vyote vinahitaji chanzo cha intaneti (router ya Vodacom, Airtel, Halotel, Tigo au fiber). Wewe utapata chanzo chako cha mtandao kisha mfumo wetu utausambaza kwa wateja.
Ndiyo kabisa. Mifumo yetu ina uwezo wa kupanuka. Unaweza kuongeza access points za ziada kufunika eneo kubwa zaidi.